Saturday, April 28, 2012

BASI LA LA COAST LINE LAPATA AJALI MKOANI MANYARA LIKITOKEA ARUSHA KWENDA DODOMA


Na Wilberd Kiwale
Simanjiro-Manyara


Hili ni basi la Coast line ambalo limepata ajali leo Juma mosi asubuhi katika kijiji cha Terrat kilichopo wilayani Sianjiro Mkoani Manyara,likitokea Arusha likielea Dodoma.



Zaidi ya abiria hamsini wamenusurika kufa baada ya basi la kampuni ya Coast line  walilokua wakisafiria kutoka mkoani Arusha kuelekea Mkoani Dodoma   kupasuka tairi  na kugonga mti katika kijiji cha Terrat Wilayani Simanjiro  mkoani Manyara.

Dereva wa gari hilo  aliyejitambulisha kwa jina la Ramadhani Musa  ambaye amevunjika mguu amesema Ajali hiyo imetokea  ghafla baada ya moja ya magurudumu ya mbele ya basi hilo kupasuka wakiwa katika mteremko  hali  iliyomfanya kushindwa kuhimili usukani na kugonga  mti uliokuwa pembeni mwa bara bara hiyo.



           Hawa ni baadhi ya abiria walionusurika katika Ajali hiyo

 

Na huu ndio mti wa Mgunga ambao Basi hili la COAST LIME limeugonga baada ya Kupasuka magurudumu ya mbele.

No comments:

Post a Comment