Saturday, February 25, 2012

ZIARA YA WAZIRI MKUCHIKA SUKURO>

SUKURO-Simanjiro,
Na Baraka Ole Maika.

Mgogoro wa kugombania Kitongoji cha Katikati baina ya Kijiji cha Sukuro na Kitiengare Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara imechukuwa sura mpya wakati wa Ziara ya Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mh George Huruma Mkuchika.

Hali ya Mtafaruku iliibuka pale Waziri Mkuchika alipoelezea kuwa Kitongoji cha Katikati kinapaswa kupiga kura na kuchagua kuwa iwepo kwenye Kijiji gani Kati ya Sukuro(Kijiji Mama) na Kitiengare(Kijiji kipya) tofauti na Awali ambapo Kitongoji hicho kilikuwa Kijiji ch Sukuro katika Taarifa iliyotolewa na TAMISEMI 2009 na kusomwa Kijijini Sukuro na aliyekuwa Mkuu wa Manyara Henry Daff Shekifu.

Taarifa hiyo ya Waziri Mkuchika iliibua hali ya taharuki na Makelele kutoka kwa wakazi wa Vijiji hivyo viwili ambao walikuwa wakimtaka Mh Waziri kutolea Maamuzi Jambo hilo kwani ndio njia pekee ya kuondoa Mvutano huo uliodumu kwa Muda sasa Kijijini hapo.

Kelele za Wakazi hao zilibainisha kuwa ni ni vema Waziri Mkuchika atolee Maamuzi jambo hilo kwani anayewavuruga na kuwakosesha usuluhishi ni Mh Christopha Ole Sendeka kwa maslahi yake Binafsi na amekuwa akifanya ziara zake Kijijini hapo pindi tu Viongozi wa Ngazi za Juu wanapofika Katika Kijiji hicho cha Sukuro.

Kelele hizo zilimfanya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Elaston Mbwilo asimame na kuwaomba wananchi hao kufuata Maelekezo waliopewa kwani Ugawanyaji wa Vijiji sio Msahafu wala Biblia ambayo haibadilishi ila Wakazi wa Kitongoji cha Katikati wakapige kura ya Kuamua kuwa waende Kijiji gani.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Manyara aliwaelekeza wakazi hao kuwa Maamuzi yao yote yaanzie Mkutano Mkuu wa Kitongoji halafu Mkutano wa Kijiji,Mkutano wa Kata(WDC),Baraza la Madiwani na Hatimae Kamati ya Ushauri ya Mkoa(RCC).

Naye Waziri Mkuchika aliwaeleza wananchi hao kuwa Mchakato huo unapaswa uwe umekamilika kabla ya Mwezi wa April na kupelekwa Ofisini kwa Waziri Mkuu.

Wakazi hao pia walimkataa Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Khalid Mandia na Mbunge Ole Sendeka kuhusika katika Mchakato huo kwa kile kinachodaiwa kuwa walishindwa tangu Mwanzo kuutatua Mgogoro huo na Sendeka ndiye Mchochezi Mkuu.

Kutokana na Kauli hiyo ya Wakazi hao Mkuu wa Mkoa wa Manyara Elaston Mbwilo alimpendekeza Mkurugenzi wa Wilaya ya Simanjiro Alhaji Mohammed Nkya pamoja wa wengine atakaowateuwa kutoka Ofisini kwake kusimamia Zoezi hilo la Upigaji kura katika Kitongoji cha Katikati.

Hali kwa kweli bado ni tete katika Vijiji vya Sukuro na Kitiengare Juu ya Kitongoji hicho cha Katikati kwani hapo awali Kitongoji hicho kilikuwa Kijiji cha Sukuro ila Wakazi wa Kitongoji hicho waligawanyika na kutokea makundi mawili ambao ni wale walioridhia kubaki Sukuro na Kundi la wale wanaotaka wawe Kitiengare.

Monday, February 20, 2012

ORBOMBA-LONGIDO 20/02/2012,
Na Baraka Ole Maika.

Vijana wa Rika la Irkiponi maarufu kama Korianga Wilayani Longido wamemzawadia Kiongozi wao wa Mila Alaiguanani Sarimu Alais Pikipiki yenye thamani ya Shilingi Milioni tatu kama usafiri utakaomrahisishia utendaji wake wa Kazi kila siku.

Wakiongea na Waandishi wa Habari Mara baada ya Kumkabidhi Kiongozi huyo Pikipiki Mmoja wa Waratibu wa Ununuzi wa Pikipiki hiyo Bw Sonjoi Ole Ndiya amesema kuwa wameamuwa kumnunulia Kiongozi huyo pikipiki kama ishara ya Mema aliowatendea,kuthamini Mchango na Uongozi wake Uliotukuka.

Aidha Bw Sonjoi amesema kuwa waliridhia hatua hiyo ya kumnunulia Alaiguanani Pikipiki ili aweze kupata Usafiri wa uhakika wa kufikia Maeneo yake yote ya Utendaji kwa Wakati kwa kutumia Usafiri wake huo hivyo kuondokana na tatizo la Usafiri ambao ulikuwa unamkwamisha kufika katika Vikao kwa wakati.

Bw Sonjoi amesema kuwa pamoja na Kiongozi huyo ktokuwa na Usafiri kwa Siku za nyuma lakini hajawahi kulalamika wala kukataa tamaa kuhudhuria Vikao mbali mbali zinazohusu rika lake na hata jamii bali wakati mwingine alilazimika kutumia gharama zake bila kujali Umbali wala Mazingira.

Aliyemkabidhi Kiongozi huyo Pikipiki kwa Niaba ya Irkiponi wote ni Bw Joseph Lankoi Ole Niini ambaye aliwashukuru sana Vijana hao kwa Tendo hilo ambalo linaonesha kuwa nao wanayathamini yale yote Mema waliotendewa na Kiongozi hiyo wa Mila.

Bw Ole Niini aliwaasa Pia Viongozi na Rika hilo la Irkiponi kudumisha Umoja,Upendo na Ushirikiano pamoja na kusaidiana na hata kuwarejesha wale wote waliotoweka na kukimbilia Mijini.

Bw Ole Niini pia alitoa kiasi cha shilingi Laki 1 ikiwa ni Mchango wake kwa ajili ya Mafuta ya Piki piki hiyo.

Awali kabla ya Alaiguanani kukabidhiwa Piki piki hiyo alibarikiwa na Wazee Mashuhuri na  pamoja viongozi wa Mila ikiwa ni tukio la pili baada ya Kiongozi huyo Kunywa Maziwa Usiku pamoja na Morani Wengine zaidi ya 30.

Mara baada ya Tukio la kukabidhiwa piki piki kukamilika Wazee waliwabariki Vijana wote kwa Maziwa ishara ya kuwatakia Mema na Baraka katika Maisha yao.

Alaiguanani Sarimu Alais aliwashukuru sana wote waliohusika katika kumpatia yeye Piki piki japo hakuwahihusita wala kuchoka kutenda yale yote yalio Majukumu yake hata kwa gharama zake na kuahidi kuwa sasa ndio atatenda kwa Ufanisi Zaidi tofauti na Awali.

Alaiguanani Sarimu ni Kiongozi wa Kwanza wa Mila kuzawadiwa Zawadi ya Usafiri(Piki piki) na Rika lake kwani tukio kama hilo haijawahi kutokea kwa Miaka ya nyuma zaidi ya Kuzawadiwa Ng'ombe,Mbuzi,Kondoo au Blanket.

 
LONGIDO,19/02/2012.
Na Baraka Ole Maika.


Rais Jakaya Kikwete amezindua Mradi wa Serikali wa Uwezeshaji Mifugo kwa Kaya zilizoathiriwa na Ukame Msimu wa 2008/2009 na 2009/2010 katika Wilaya za Longido,Monduli na Ngorongoro.


Uzinduzi wa Mradi huo utakaogharimu shilingi 11.2 Bilioni ulifanyika katika Uwanja wa Mnadani Wilayani Longido Mkoani Arusha na Kuhudhuriwa na Viongozi mbali mbali wa Mila Chama na Serikali pamoja na Wakazi wa Wilaya ya Longido waliofurika kwa Wingi katika Eneo hilo kushuhudia tukiohilo la Kihistoria.


Akihutubia hadhara hiyo Rais Kikwete aliliwataka Wafugaji wa Longido na Wilaya Zingine zitakazonufaika na Mradi huo kutambua kuwa hiyo sio fidia ila ni huruma tu ya Serikali kwa hakuna aliyesababisha Ukame ulioteketeza Mifugo hao ya Wafugaji.

Aidha Rais Kikwete aliwakabidhi Mifigo hao baadhi ya Waathirika kutoka Kata 16 na kuiwaasa Wafugaji kuwa wajifunze kufuga Mifugo wachache wenye Tija kwao na wataomudu kuwahudumia kulingana na Maeneo waliopo na pia kwa kuangalia hali ya Mazingira na Maeneo waliopo.

Pamoja na Hayo Rais Kikwete aliawataka Wananchi hao washiriki kikamilifu katika Zoezi la Sensa ya Watu litakalofanyika August'2012 na kujiokeza kwa wingi katika utoaji Maoni ya Kuunda Katiba Mpya inayotarajiwa kukamilika kabla ya Mwaka 2015.

Kuhusu tatizo la Maji katika Wilaya ya Longido hasa Longido Mjini Rais Kikwete aliwaomba Wakazi hao wawe na subira wakati akilitafutia ufumbuzi tatizo hilo.


Rais Kikwete pia aliwaasa Wafugaji wote waliopata Mifugo kupitia Mradi huo kutotumia Mifugo hao kwa Matumizi yaliyo kinyume na Lengo lililokusudiwa.


Naye Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mh Mathayo David aliwaeleza Wananchi hao Mikakati ya Serikali katika kuboresha Uboreshaji wa Mifugo ili ziweze kuleta tija kwa Mfugaji kwa ndio njia pekee ya Kiuchumi inayotegemewa na Wafugaji.


Viongozi Mbalimbali walioandamana na Mh Kikwete katika Ziara yake hiyo ni Pamoja na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu na Bunge Mh Wilium Lukuvi,Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mh Mathayo David,Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mh Benedict Nangoro,Mbunge wa Monduli Mh Edward Lowasa,Saning'o Telele(Ngorongoro),Mbunge wa Karatu na Mbunge wa Longido Mh Michael Lekule Laizer.


Wengine walioshudia Uzinduzi wa Mradi huo ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo,Mkuu wa Wilaya ya Longido Jamsi Milya,Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mercy Silla,Mkuu wa Wilaya ya Monduli Jowika Kasunga,Mkuu wa Wilaya ya Karatu Sedeyeka na Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Wawa Lali.


Mradi huo wa kuwawezesha Wafugaji waliopoteza Mifugo yao wakati wa Ukame 2008/2009 ni wa Kwanza kufanyika Tanzania na utanufaisha kaya Zaidi ya Elfu 7 kutoka Wilaya za Longido,Monduli na Ngorongoro kwa kila kaya kupatiwa Mitamba minne na Dume moja isipokuwa Wilaya ya Longido ambao wao wameomba wapatiwe Mitamba Mitano,ila Pamoja na Mitamba hiyo kuna baadhi ya Kaya watapatiwa Mbuzi watano.

Friday, February 17, 2012

Longido leo Jioni.


Longido.
Na Mwandishi wetu, 
Baraka Ole Maika.
Kiongozi wa Rika la Irkiponi(Korianga) Wilayani Longido Alaiguanani Sarimu Alais atawaongoza Vijana zaidi ya 40 wa rika hilo katika sherehe ya kunywa Maziwa(Ewokoto E kule) siku ya Leo Jioni katika Kitongoji cha Emamra Kijiji cha Orbomba Wilayani Longido.

Sherehe hiyo inatazamiwa kuhudhuriwa na Viongozi mbali mbali wa Mila,Chama na Serikali kutoka Maeneo mbali mbali ya Wilaya ya Longido na Maeneo ya Jirani.

Alaiguanani Sarimu atasindikizwa na Vijana zaidi ya 40 wa Rika la Irkiponi katika Unywaji wa Maziwa ikiwa ni hatua Muhimu kwa Kila Rika ndani ya Jamii ya Kimaasai ambayo inatoa Fursa kwa Kiongozi wa mila na Rika lake kuingia katika Maandalizi ya Kuelekea Uzeeni(Orng'ehher) na Kuwapa Madaraka Rika Jipya la Iltubula almaarufu kama Nyangulo.

Hatua hii inafikiwa kila baada ya Miaka 15 hadi 20 ambapo Rika la Vijana lililokuwa Madarakani linaachia nafasi Rika jipya lililoandaliwa kwa Miaka 20 iliyopita tayari kupokea madaraka ya Ulinzi na Usalama wa Jamii na Mifugo yao.

Wednesday, February 8, 2012


TERRAT SIMANJIRO-20120702Swaa.doc.jumanne

Semina ya siku mbili ya mafunzo elekezi ya upashanaji habari za kijamii imeanza leo katika ukumbi wa mikutano wa taasisi ya shirika la Ilaramatak lorkonerei uliopo Terrat Simanjiro mkoani Manyara

Wakizungumzia lengo la mafunzo hayo wawezeshaji ambao ni bwana Moses Ndiyaine na Lucas Ole Kariongi wamesema jamii inapaswa kutambua na kupata fursa ya kuchangia maendeleo yao katika kila jambo linalo wahusu

Mafunzo hayo yanawalenga watumishi wa Orkonerei Mass Media na wanahabari wote wa O.r.s fm  kwa lengo la kufanikisha majukumu yao ya kila siku ya kuhabarisha jamii juu ya mambo mbali mbali yanayotekea katika jamii hapa nchini.

Wawezeshaji hao wamewataka wanahabari kuandika habari mbali mbali za jamii ikiwamo unyanyasaji wa wanawake upatikanaji wa huduma muhimu kama hospitali shule bara bara na masuala yanayo wahusu watoto na haki zao

Nao watumishi waliohudhuria warsha hiyo wameahidi kutekeleza mafunzo hayo wanayopewa na pia kufuata kanuni,sheria na taratibu za uandishi wa habari